Tuesday 8 December 2015

MBINGA YA ADHIMISHA SIKU YA UHURU KWA KUTEKELEZA AGIZO LA USAFI

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga imetekeleza agizo la usafi kwa siku ya uhuru kama lilivyotolewa na Mh. Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Mheshimiwa Joseph Pombe Magufuli.
Aidha katika kufanikisha  hilo, Wilaya ilitumia mbinu shirikishi kwa kuwatumia wadau mbali mbali wakiwemo wafanyabiashara , taasisi za kifedha , mashule na vikundi mbali mbali.

Ufanya usafi kwenye mazingira yetu unafaida nyingi,kunasaidia kuepukana na magonjwa yanayotokana na uchafu. Magonjwa kama kipindu pindu , minyoo, kichocho na maralia kwani mbuu huzaliana katika mazingira ya uchafu.



 PICHA: Kijiko kilichotolewa na Kanisa Katoliki jimbo la  Mbinga Kikisaidia upakiaji wa taka taka katika roli la halmashauri  dampo la misheni.Mji wa Mbinga na vitongoji vyake umekuwa katika hali ya usafi baada ya kampeni hii ya usafi.

No comments:

Post a Comment